Duka la Mavazi ya Kisasa na yenye hadhi ya Kimataifa la J&M Virgo linasherehekea Mwaka mmoja toka kuanza kwake,huku likitoa shukrani nyingi kwa wateja wake na wadau mbali mbali,ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa ni sehemu ya mafanikiwa kwa Duka hili kufikia hapo walipo sasa.Pamoja na kusherehekea kwao Mwaka mmoja tangu kufunguliwa kwa Duka hilo,pia wameleta mali mpya kibao toka USA,Italy,UK na Turkey kwa ajili ya msimu wa Sikukuu za Krismass na Mwaka Mpya.
 Wakurugenzi wa Duka la Mavazi la J&M Virgo,James na Mishy wakikata keki iliyoandaliwa kwa ajili ya hafla fupi ya kusherehekea Mwaka mmoja wa Duka lao hilo toka lianzishe,iliyofanyika Dukani kwao hapo,Mikocheni kwa Warioba,jijini Dar ndani ya jengo jipya la C&G Plaza.Pamoja na kusherehekea kwao Mwaka mmoja tangu kufunguliwa kwa Duka hilo,pia wameleta mali mpya kibao toka Ughaibuni kwa ajili ya msimu wa Sikukuu za Krismass na Mwaka Mpya.
Wakurugenzi wa Duka la J&M Virgo,Da' Mishy (kulia) na Mdau James (pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na timu yao nzima,huku wakiwa wamepigilia pamba za nguvu ambazo ni sehemu ya mzigo mpya ulioingia hivi karibuni Dukani hapo,Mikocheni kwa Warioba,jijini Dar ndani ya jengo jipya la C&G Plaza,ambapo sasa wapo na ofa ya msimu wa Krismas na Mwaka mpya.Fika dukani kwao hapo na ujipatia vitu vya ukweli.
Magauni makali kwa kina dada.
Moka za ngunu kwa kina Baba.
Michuchumio ya uhakika kwa kina Dada.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Thanks, we ladies needs flat shoes also, and dresses for big mamas.

    thanks

    ReplyDelete
  2. Punguza mwili. kama hayo magauni walovaa wamiliki hayakutoshi jua you are in trouble....fanya mazoezi dear

    ReplyDelete
  3. You made me laugh, "dresses for big mamas".

    ReplyDelete
  4. what's fanny my dear even big mamas are good , sweet and nice

    ReplyDelete
  5. naomba nr ya simu au e mail ya hili duka tufanye biashara au niandikie e mail yangu

    z.nz@hotmail.com

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...