Afisa habari Ngazi ya Taifa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma akitoa maelezo ya awali kuhusiana na mafunzo hayo yanayolenga kuwawezesha vijana kuwa na uelewa na mbinu juu ya ujasiriamali na namna ya kusimamia biashara zao ili kuongeza uzalishaji hivyo kupambana na kuupunguza umasikini katika ngazi zao kabla ya kumkaribisha Mratibu wa Taifa wa Mradi wa ILO wa Ujasiriamali kwa vijana Bw. Louis Mkuku (kushoto).

Ameongeza kuwa pamoja na kupata uelewa juu ya ujasiriamali mafunzo hayo yanakwenda sambamba na lengo namba 1 la Maendeleo ya Milenia ambalo ni Kupunguza Umasikini, kwa kuwa yatawapatia mbinu zitakazowawezesha kuboresha shughuli zao za kujipatia kipato hivyo kuwa na kipato endelevu.
Mratibu wa Taifa wa Mradi wa ILO wa Ujasiriamali kwa vijana Bw. Louis Mkuku akifungua rasmi mafunzo hayo ambapo ametoa hamasa kwa vijana kutumia vizuri elimu watakayoipata wakati huu wa ujana wao kujenga maisha ya baadae na kuahidi kufuatilia kwa umakini matokeo ya mafunzo hayo na kusema atahakikisha kila mwenye ndoto itatimia kwa usimamizi wa ILO na UNIC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...