Mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Mgune Masatu akitoa maoni yake kuhusu katiba Mpya katika mkutano wa Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa kutoa maoni yao uliongozwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Peniel Lyimo (Hayupo pichani). Mkutano huo umefanyika kwa muongozo wa Tume ya mabadiliko ya Katiba ili kuwapa nafasi watumishi wa Umma kutoa maoni yao kwa kuwa wakati Tume hiyo ilipo kuwa ikikusanya maoni kwa wananchi wa kawaida watumishi wengi wa Umma walikuwa maofisini, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu leo, Jijini Dar es Saaam.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakitoa maoni yao kuhusu katiba mpya kwa njia ya maadishi kwa kunukuu vipengele muhimu vya kuchangia kutoka katiba ya sasa wakati wa mkutano wa Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa kutoa maoni yao, (wa kwanza Kushoto) ni Bw. George Biligwija, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu leo, Jijini Dar es Saaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...