Waziri wa  Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Mh. Dkt. Fenella Mukangara (mwenye miwani ) leo amepokea taarifa ya kikundi cha Petu Saccos na kuongea na  vijana wa kikundi cha Youth Welding Group cha Sanawari  - Arusha (pichani) alipotembelea na kuangalia jinsi fedha za mfuko wa vijana zilizotolewa  wizara yake zilivyowanufaisha  vijana katika kujikomboa kimaisha na kujiajiri wenyewe.

 .Waziri  wa Habari , Vijana, Utamaduni na Michezo  Mh. Dkt. Fenella Mukangara (alivaa miwani ) akiongea na wana Saccos wa Petu kupitia kikundi cha Youth Welding group cha Sanawari  mkoani Arusha leo

 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na .  Michezo Dkt. Fenella Mukangara (kushoto)leo akizungumza na Mjasiriamali Martha  Yusuph alipotembelea  Soko kuu Saccos Arusha na kuangalia wanufaika wa mikopo ya mfuko wa vijana uliotolewa na Wizara yake
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara (kulia) akipata maelezo kutoka kwa mjasiriamali wa  Krokon Saccos Asha Muhamed jinsi alivyonufaika  mkopo wa mfuko wa Vijana kutoka Wizara yake .

Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo, Mh. Dkt. Fenella Mukangara (alievaa miwani) akiongea na wafanyakazi wa  TBC na Mafundi wa Star Times leo alipotembelea  Njiro mkoani Arusha  kuangalia shughuli mbalimbali. Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. madogo wa welding wanajitahidi, wangepata marketing tools ingekua poa zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...