Picha Zote zinaonyesha Washiriki wa Miss Utalii Tanzania wakiwa wanatembelea Ukumbi wa Kimataifa wa Makumbusho ya Taifa(NATIONAL MUSIUM THEATRE).
Washiriki wa Fainali za Taifa za mashindano ya Miss Utalii Tanzania 2012/13,jana wametembelea Ukumbi wa kwanza na wa Kisasa na wa aina yake Tanzania ambao unamilikiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia kurugenzi ya mambo ya kale na makumbusho ya Taifa uliopo ndani ya Makumbusho ya Taifa jirani na Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM) karibu na maeneo ya Ikulu jijini Dar es Salaam.
Wakiwa katika Ukumbi huo wenye uwezo wa kuchukua watu 470 kwa wakati mmoja, walishuhudia Viti,Mitambo na vifaa vingine vya kisasa vyenye uwezo wa kuendesha Matamasha na mashindano ya Urembo kwa kiwango cha hadhi ya nyota tano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...