Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akifafanua Jambo wakati alipotembelea Mradimpunga wa Umwagiliaji kwenye Bonde la Mpunga la Jendele kulia Mwenyekiti wa Tasaf Jendele Ali Mussa waziri alifanya Ziara ya Wilaya ya Kati Unguja kukutembelea Mradi Uliofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mratibu wa wa Programu ya kuimarisha huduma za kilimo Bw Zaki Khamis Juma akimueleza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan kuhusu wakulima wa kuzalisha Mbegu za Mpunga kwenye Bonde la Kinyasini -kisongoni Wilaya ya Kaskazini A Unguja wakati wa Ziara ya kutembelea Miradi ya Tasaf na Assp inayofadhiliwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akipita kwenye shamba la mpunga la kuzalishia Mbegu la kinyasini-kisongoni Walaya ya Kaskazini A Unguja Waziri akiwa katika Ziara ya kutembelea Miradi iliyofadhiliwa na ASSP. Picha na Ali Meja.
Na Ali Issa, Maelezo, Zanzibar
Waziri wa nnchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Mhe Samia
Suluhu Hassan amesema kuna umuhimu
mkubwa kwa wananchi kuituza na kuindeleza miradi inayo fadhiliwa na Serikali
zote mbili na washirika wa maendeleo ili
miradi hiyo iendelee kuwanufaisha na kutimiza lengo lililokusudiwa.
Hayo ameyasema huko Jendele wilaya ya kati Mkoa wa Kusini
Unguja wakati alipo fanya ziara
kutembelea miradi mbali mbali ya kilimo iliyofadhiliwa na TASAF kupitia
Serikali ya Muungano wa Tanzania .
Amesema Serikali imekua ikitoa pesa nyingi kufadhili wananchi
katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo kwalengo kwamba wananchi hao waweze
kujikwamua na umasikini na kujipatia kipato jambo ambalo baada ya mradihuo
kukabidhiwa wananchi husuasua na hatimae kufa kituambacho hakifurahishi.
Amesema wana nchi wajifunze kuituza na kuendeleza miradi
hiyo kwani ina umuhimu mkubwa na kuwanufahisha wao wenyewe. “Kuiacha miradi ife si vizuri. Muichangie
iliijiweze kujiendesha na hiyo ndiyo faida ya miradi hiyo”.alisema Samia.
Aidha Waziri aliwambia wakulima wa bonde la Jendele, Kinyasini
na Kisongoni wajitume kwa kuzalisha kwa
wingi chakula kwani sasa hakuna sababu kwavile maji yapo ya kutosha katika
bonde hilo
hivyo uzalishaji ungezeke.
Waziri huyo alisema dhamira ya ziara yake kuja Zanzibar ni kuona vipi
matumizi ya pesa za TASAF zinavyo tumika katika miradi ilio ombewa na
utekelezaji wake umefikiaje kwa wananchi. Alifurahishwa na juhudi zinazochukuliwa
kwani kumefikiwa hatua kubwa za kumaendeleo na zinatia moyo kwa matumaini .
Waziri alitembelea mradi wa
mpunga wa umwagiliaji maji jendele na mradi wa uzalishaji mbegu za
mpunga Kinyasini na Kisongoni na baadae kupata maelezo juu ya miradi ASSP na
SPDL inayo endeshwa na wizara yakilimo na maliasili na ushirika Zanzibar .
Miradi hiyo kwa TASAF ya awamu ya kwanza Zanzibar
ilipatiwa dola za kimarekani milioni tatu ambapo ziligawiwa sawa sawa
kwa Unguja na Pemba.
Awamu ya pili TASAF Zanzibar ilipatiwa dola za kimarekani
2,500.000.00 ambapo zilitumika kumalizia
mradi wa kwanza Unguja na Pemba kupitia mfuko wa Taifa wa kijiji (NVF) wenye thamani
ya fedha TShs 2,500,000,000.00,mfuko wa mradi wa ukanda wa Bahari (MACEMP)
wenye thamani ya fedha TShs 1,800,000.000.00
Ziara hiyo itaendelea kwa kutembelea idara ya uhamiaji Zanzibar na malaka ya kitambulisho cha Taifa
Zanzibar.
Nimekuvulia kofia mama, kweli wewe kiongozi hata tope hujali!
ReplyDeleteHawa ndo kati y viongozi wachache tulionao ambao hawajitangazi lakini wako committed.
ReplyDeleteBig up mama!!!
Nashukuru sana Mama kwa mfano wako mzuri. Hawa ndiyo Mawaziri tunaowataka sisi Watanzania. Wenye kujituma kwenda kule wanakoishi Watanzania halisi wanaohitaji kusaidiwa.
ReplyDeleteMwenyezi Mungu na azidi kukupandisha Mama yangu.
kwani hakujua kuwa atakutana na kaka/dada tope?
ReplyDelete