Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) aliyemwagiwa Tindikali na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa pili kulia Kaka yake Sheha Sudu Mgeni Saidi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimuangalia Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) jinsi alivyoathirika na Tindikali alilomwagiwa na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa kushoto Dk.Slim Mohamed Mgeni,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 25, 2013

    Sijui kwanini jamani lakini watu wanafanya hivi, walau basi waseme wanataka nini ili ijulikane kuliko kuumiza watu.Kuweni wazi mnataka nini??

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 25, 2013

    ubinaadam haupo tena ila umebaki unyama. mimi nadhani kuwekwe sheria kali kwa wakosaji kama hawa sio kuwanyoa ndevu tu na baadae kuwapa dhamana. inatakiwa akipatikana basi na yeye amwagiwe tindikali.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 26, 2013

    hahaaaa anony no 2 unasahau yesu amesema nini? ukipigwa kofi shavu upande mmoja basi mgeuzie na shavu la upande wa pili akupige , sasa hii tindikali kwa tindikali imetokea wapi?

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 26, 2013

    kwa hiyo aegeshe shavu lingine hilo amwagiwe tindikali ....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...