Kikosi cha Taswa Fc, TIMU ya Taswa Fc jana iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya timu ya Full Mabondia, inayoundwa na mabondia mahiri wa Jijini Dar es Salaam. Timu hizo zilikutana katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar jana mchana, huku timu ya mabondia ikiwakilishwa na mabondia kama, Thomas Mashali, Mchumiatumbo, Francis Miyeyusho, Majia, Kanda Kabongo, na wengine wengi. Picha zote na www.sufianimafoto.com
 Beki wa Taswa Fc, Juma Ramadhan, (nyuma) akimdhibiti mshambuliaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo.
 Beki wa Taswa Fc, Muhidin Sufiani 'Sufianimafoto' (kulia) akimfinya mchezaji wa Full Mabondia, wakati wa mchezo huo jana.
 Beki wa Taswa Fc, Elius Kambili, akiambaa na mpira.
 Beki wa Taswa Fc, Salim (kulia) akiondosha moja ya hatari mbele ya Bondia, Mchumiatumbo.
 Kipa wa Full Mabondia, akiwa golini huku akiwa peku peku, wakati wa mtanange huo jana.
 Zahoro Milanzi wa Taswa Fc, (kushoto) akiambaa na mpira wakati wa mtanange huo.
 Wachezaji wa Taswa Fc, wakipasha kabla ya kuanza kwa mtanange huo jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Geofrey ChambuaMay 20, 2013

    inakuwaje kipa pekee ndoye hana viatu?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 21, 2013

    Vitambi hivyo mkianguka mna insurance?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...