Ujumbe wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) uko nchini Rwanda kubadilishana ujuzi na uzoefu na Rwanda kuhusu utekelezaji wa mradi wa kurahisisha na kuwezesha biashara (Trade Facilitation) kwa kutumia TEHAMA - Electronic Single Window System. Muda mfupi ujao TPA itaanza utekelezaji wa mradi huo kwa niaba ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji, Forodha, wafanyaniashara na wadau wote wa Tanzania. Ujumbe huo wa Tanzania unaongozwa na Mkuu wa mradi na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya TEHAMA-TPA Ndg. Phares Magesa wa kwanza kushoto, wengine ni Mathayo Ntandu, Jesse Shali na Kilian Chale ambao ni maofisa wakuu TPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 23, 2013

    kwa aibu kabisa tunakwenda kujifunza Rwanda na bado tunachekelea tu. Single Window System imeimbwa miaka mingapi leo hii ndio mnaenda kujifunza Rwanda?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 23, 2013

    mbona muonekano wa nchi za wenzetu ni safi sana na hata kama wana mji mdogo lakini muonekano wa kisasa na wenye unafasi na sio bongo yetu kujibana kwa kwenda mbele na machafu machafu kibao

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 24, 2013

    Hapo Rwanda kweli au Ulaya Ankal?? Haiwezekani iwe Rwanda. Hawa jamaa walikuwa kwenye vita kwa muda mrefu tu? Hivi Tanzania mbona haipo safi hivi?

    ReplyDelete
  4. enhee naratajia nyote mliochangia mwanzo ni Watanganyika sasa semeni wenyewe hii ni haki?

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 24, 2013

    chezea Phares magesa ww, this guy is very strutagic. town guy

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...