.Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako  Manongi akiwa  na Mkuu mpya ya UNAMID Luteni Jenerali Paul Ignace Mella na  kulia ni Luteni Jenerali Wynjones Mathew Kisamba Naibu  Kamanda na ambaye pia alikuwa akikaimu nafasi ya Kamanda Mkuu UNAMID. Luteni Jenerali  Mella na Luteni  Jenerali Kisamba walikuwa hapa  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwa  ziara ya Kikazi na mafunzo. Lt. Jenerali Mella   anasema yupo tayari kulitekeleza jukumu alilokabidhiwa na Umoja wa Mataifa na  kwamba  uteuzi wake katika wadhifa huo ni heshima kubwa wa Tanzania,  Afrika, kwake yeye binfasi na zaidi kwa JWTZ ambayo mwaka itakuwa inatimizia miaka 50  tangu kuanzishwa kwake
 Wageni waalikwa wakipata kitu kidogo.
 Mkuu Mpya wa UNAMID Luteni Jenerali Mella akiwa katika picha ya pamoja na waambata wa kijeshi kutoka nchi za Afrika na  kwingineko wakati alipotambulishwa kwao katika hafla fupi iliyoandawali na  Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. kutoka  kushoto ni  Naibu Mwakilishi Balozi Ramadhan Mwinyi,  Lt. Jenerali Wynjones Kisamba,  Balozi Tuvako Manongi,  Lt. Jenerali Paul Mella na  Maj.  Jenerali Ngodi Mkuu wa jeshi la kulinda amani huko Lebano (UNFIL)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...