Afisa uhusiano wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) Dollah Kilo akifurahia jambo na naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge wakati akitembelea tangi la maji la kampni ya maji ya Kiliwater wilayani Rombo.
Tangi la maji la Kampuni ya Kiliwater linalohifadhi maji kwa ajili ya wakazi wa wilaya ya Rombo.
Naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge akipanda katika ngazi ya tangi la maji la kampuni ya Kiliwater kujionea hali ya ujazo wamji ikoje katika tangi hilo.
Naibu wziri wa maji Dk Binilith Mahenge akizungumza na watendaji wa maji wilaya ya Rombo juu ya tangi la maji la kampuni ya Kiliwater.
Naibu wziri wa maji Dk Binilith Mahenge akitizama sehemu ya kuchanganyia dawa katika tangi la maji la kampuni ya maji la Kiliwater.
Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na maji safi mjini Moshi Cyprian Luhemeje akiongea jambo mbele ya naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge mara baada ya kutembelea miradi ya maji katika wilaya ya Rombo. Picha na Dixon Busagaga wa globu ya jamii ,Moshi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 30, 2013

    Mhe. Dr. Mahenge kweli kazi anaiweza,

    Maana wachakachuaji hawaishi Mipango, ukitegemea kupokea taarifa kwa njia za simu utaula wa chuya!.

    Wanaweza kupokea Madawa ya kusafishia maji tani 15 kwenye makaratasi wakaandika tani 1.5 halafu mzigo mwingine wanaupeleka huko Miferejini Keko na Manzese.

    Mzee mzima hadi anapanda ngazi kuhakikisha?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 30, 2013

    Mbongo ni kama Kima, ukicheza naye utavuna mabua.

    Ndio maana Mhe. Dr. Mahenge haamini taarifa za kwenye makabrasha hadi apande ngazi ahakikishe mwenyewe!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 30, 2013

    Ama kweli seeing is believing!

    Ndio maana Kiongozi Dr.Mahenge anapanda ngazi kuhakikisha yeye mwenyewe.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 30, 2013

    Ama kweli seeing is believing!

    Ndio maana Kiongozi Dr.Mahenge anapanda ngazi kuhakikisha yeye mwenyewe.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 30, 2013

    Nyinyi mnaparamia kwenye matanki hayo ninyi "Mtaporomoka" humo halafu mkione cha mtema kuni.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 30, 2013

    waziri huyu anafanya kazi sana bila wasiwasi...wangekuwa kumi hivi..tungefika mbali...

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 31, 2013

    Hapa wachapakazi hawatakiwi bongo. Angalia mashirika ya umma yalikufa kwa sbb wachapakazi aidha walifukuzwa kiaina ama walinyanyaswa wakaacha kazi.

    Ndio maana Tz inaongozwa kiujanja si kisayansi.

    Hebu ona.. UCC ya Mlimani ilikuwa murua sana wakati wa Prof. Beda kiutawala. Na uhasibu kulikuwa na mama mmoja jina limenitoka au sikuwahi kulijua.Watu hawa wawili walikuwa wachapa kazi sana.Ndio, kiubinadamu hakuna mkamilifu lakini kampuni ilisonga mbele.

    Sijui ni mchawi gani alingilia pale. Prof. wa watu silipofika pale baadaye nikasikia amechimbiwa mkwala akaondolewa. Haya...na huyu mama nikasikia hakutaka kushiriki wizi baada ya prof kuondoka, naye akanyanyaswa ikabidi aachie ngazi.

    Hebu ona kampuni inavyoyoyoma kisailensa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...