Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.

WIZARA ya mambo ya ndani ya nchi imesema imejipanga kukabiliana na mashambulio ya kigaidi kama lile lililotokea hivi karibuni katika jengo lenye maduka makubwa ya biashara la Westgate ambapo zaidi ya watu 60 wameuawa huku wengine zaidi ya 100 wakijeruhiwa vibaya.

Tukio hilo la kihistoria lililotikisa Jiji la Nairobi nchini Kenya kwa takribani siku nne limechangia pia kuwepo kwa hali ya tahadhari kwa Tanzania na sasa hofu imetanda ndani ya mikoa iliyo jirani na Kenya na hata katika maduka makubwa yanayo milikiwa na wakenya kama Nakumat lililopo mjini Moshi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa maofisa wanadhimu,wahasibu na maofisa mipango wa mikoa na vikosi wa jeshi la polisi ,naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani Mwamini Malemi alisema serikali iko tayari kukabiliana na hali yoyote ile ya kigaidi.

Alisema kutokana na tukio hilo la Kenya nchi imepata fundisho ya nini kinatakiwa kufanyika kwa sasa katika kukabiliana na hali hiyo huku akiwataka wananchi kutoa taarifa katika vyombo vya ulinzi na usalama pale wanapokuwa na shaka juu ya watu ambao hawaeleweki.

“Sisi tumejipanga unajifunza kutokana na matatizo yanayompata mwenzio kwa hiyo unachukua tahadhali kwa lile lililotokea kwa mwenzetu nafikiri tuko vizuri ,wananchi wanatakiwa wawe watulivu kwa sasa, lakini wanatakiwa kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama kwa mtu yoyote wanaye mtilia wasiwasi”alisema Malemi.
Mgeni rasmi katika mkutano wa siku tatu wa wa maofisa wanadhimu,wahasibu na maofisa mipango wa mikoa na vikosi wa jeshi la polisi ,naibu katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya chi Mwamini Malemi akiwa ameongozana na mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini Robert Manumba pamoja na mkuu wa chuo cha taaluma ya Polisi Moshi,Commandant Matanga Mbushi wakielekea katika ukumbi wa mkutano .
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwamini Malemi akizungumza katika mkutano huo.
Mhasibu mkuu wa Polisi Frank Msacky akizungumza katika mkutano huo.
Hali ya ulinzi ilikuwa ni ya hali ya juu katika eneo la CCP ambako mkutano huo umefanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...