ZAIDI ya  washiriki 100 kutoka ndani na nje ya nchi watashiriki kwenye tamasha la Sanaa na utamaduni la Jambo Festival litakalofanyika oktoba 23 hadi 27 mwaka huu katika viwanja vya Suye vilivyopo Arusha.


 Mwenyekiti wa tamasha hilo, Augustine Namfua alisema kuwa tamasha hilo ni la pili kufanyika mkoani Arusha ambapo wamekuwa wakifanya kila mwaka lengo likiwa ni kuwawezesha  washiriki mbalimbali kuweza kuonyesha bidhaa zao za kitamaduni kutoka ndani na nje ya nchi.


Alisema kuwa tamasha hilo la kimataifa pia litawashirikisha washiriki kutoka nchi za Ufaransa na Angentina ambao wataonesha mambo mbalimbali na kuonyesha bidhaa zao za kitamaduni  .


Alisema tamasha hilo litaenda sambamba na matukio mbalimbali ya kiasili ikiwemo maonyesho  ya mavazi ya kiasili, pamoja na tamasha la kiasili kutoka vikundi  vya miji ya  Tanga, Arusha,  na Dar es Saalamu .

 Namfua aliongeza pia kutakuwepo na tamasha la muziki wa kisasa    pamoja na onesho la  mavazi, na ubunifu wa mavazi ambapo  kwa siku hizo kila siku kutakuwa na matamasha mbalimbali.


 Amesema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kwa asilimia 50 huku watu mbalimbali wakiwemo watu binafsi, mashirika na taasisi mbalimbali zinazohusika na maswala ya sanaa na tamaduni wanaendelea kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kushiriki.


 "Tamasha la mwaka jana lilifana sana kwani tuliweza kupata washiriki wengi sana kutoka ndani na nje ya nchi na lilikuwa na mwitiko mkubwa sana , huku watu mbalimbali wakipata fursa ya kuonyesha sanaa zao na tamaduni mbalimbali na kuweza kujifunza kutoka kwa wenzetu wa nje ya nchi ndio maana tumeamua kufanya tena mwaka huu mwezi wa kumi hivyo tunatarajia  watu mbalimbali kushiriki kikamilifu katika tamasha hilo’alisema Namfua.


 Aidha aliwataka watu mbalimbali kufika katika tamasha hilo na kuonyesha  bidhaa zao za kitamaduni zinazotengenezwa kwa mikono pamoja na kutangaza tamaduni zao za Kiafrika na kuwataka wadau mbalimbali kuonyesha  moyo katika kusaidia matamasha hayo  ili yaendelee kufanyika mara kwa mara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. good job Augustine

    ReplyDelete
  2. Hongera sana Augustine.....All the best

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...