Siku, miezi na miaka imepita, leo imetimia miaka Ishirini na Tano (25) tangu Mwenyezi Mungu akuite nyumbani.

Jumatatu ile ya majonzi makuu, Bwana alitazama shambani mwake, akaona sehemu iliyo wazi. Kisha akatazama duniani, na kukuona ukiwa hoi taabani, pale hospitalini. Ndipo alipokukumbatia na kukuambia “Emmanuel, imetosha, njoo nyumbani”.

Hakika bustani ya Bwana yapendeza, maana imesheheni watu wake walio bora, wampendezaye.

Ahadi ya Bwana imetimia, kama yanenavyo maandiko matakatifu kuwa, “…Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele, wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”. Yohana Mtakatifu 5:24

Nasi tunazidi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya maisha haya, tangu tulivyokuwa nawe kimwili hadi sasa ambapo unaendelea kudumu nasi kiroho. Na imani yetu sote imezidi kuimarika.

Tena tunamshukuru Mungu kwa baraka na rehema zake zisizo kifani. Tunamshukuru kwa kutimiza ahadi zake kwetu.

Unakumbukwa sana na familia yako, ndugu, majirani na marafiki. Mama Salome, watoto wako wote na wenzi wao, wajukuu zako, dada, kaka na wengine wote wanakukumbuka, kila mmoja kwa namna ya kipekee.

Kwetu unaendelea kudumu katika kila pumzi ya uhai wetu. Tunaendelea kusimama katika misingi uliyoiweka, tena bila kutetereka. Tunakuenzi kwa vitendo, tena bila kuchoka. Ndio maana tuna kila sababu ya kusherehekea siku hii ya matumaini - tukitumaini kuwa, siku moja tutaungana nawe katika shamba la Bwana, maskani yetu ya milele.

Hadi tutakapofika huko, tunazidi kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuilaza roho yako mahala pema peponi, kwa watakatifu wake. Amen.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Judge Salome kaganda mungu akubariki

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...