MAMBO YANAENDELEA! Tamasha la wanamitindo na wabunifu walio katika vyuo vikuu lijulikanalo kama ‘Redd’s Uni-Fashion Bash’, mwishoni mwa wiki hii linatarajiwa kufanyika mkoani Kilimanjaro, baada ya Mwanza kufungua pazia.
 
Tamasha hilo linalochochea vipaji ndani ya vyuo hivyo, mbali na Mwanza na Kilimanjaro pia litahusisha vyuo vilivyopo katika Mikoa ya Dar es Salaa na Iringa.
 
Akizungumzia tamasha hilo, Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Fimbo Butallah alisema, linatarajiwa kufanyika Jumapili ndani ya ukumbi wa Glessius uliopo mjini hapa.
 
Fimbo alisema, wanafunzi wa vyuo vyote vya elimu ya juu walio na mapenzi katika ubunifu na mitindo wanatarajiwa kushiriki shindano hilo, huku akiamini kukiwa na upinzani mkali zaidi ya ule wa Mwanza.
 
“Siku zote tunaamini katika kukuza vipaji zaidi, ila siku hiyo kutakuwa na burudani kali kutoka kwa msanii Jon Makini,” alisema Butallah.
 
Katika tamasha la awali lililofanyika Mwanza, kulikuwa na ushindani mkali katika mitindo ambapo Fahad Rajab kutoka Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT) aliibuka mshindi akifuatiwa na Lucy Charles kutoka pia chuo hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...