Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha-Rose Migiro, akimpongeza Kada wa CCM, Asha Abdallah Juma, baada ya kumtunuku shahada ya pili ya Biashara ya Chuo hicho, katika mahafali ya 25, yaliyofanyika leo, Makao Makuu ya OUT, Bungo, Kibaha mkoa wa Pwani. Kushoto ni Makamnu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Tolly Mbwette. Asha ambaye sasa ni Mjumbe wa NEC CCM, amewahi kuwa Wazirikatika serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia Katibu wa NEC, Oganaizesheni.

MKUU wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma katika Idara ya Itikadi na Uenezi CCM, Makao Makuu, Daniel Chongolo, akipongezana na Mjumbe wa NEC ya CCM, Asha Abdallah Juma baada ya wote kutuniwa shahada zao katika mahafali ya 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), yaliyofanyika jana, Oktoba 27, Bungo, Kibaha mkoa wa Pwani. Chongolo ametunukiwa shahada ya kwanza ya Mawasiliano ya Umma na Asha shahada ya Pili ya Biashara. Katikati ni Kada wa CCM, Rachel Kyala ambaye pia ametunukiwa shahada ya Mawasiliano ya umma.

Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania , Dk. Asha-Rose Migiro akiteta na Makamu wake, Tolly Mbwette wakati wa mahafali hayo.
Abdallah Majura baada ya kupata shahada yake
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...