Askari polisi wakiwa na silaha wakiwa wamezingira nyumba iliyokuwa
ikitumika kwa shughuli za kutolea Mimba.
Daktari mstaafu wa hosptali ya rufaa ya Mawenzi Frances Shayo akiwa
mikononi mwa polisi muda mfupi baada ya kumkamata akitaka kuwatoa
Umati wa watu waliofika katika nyumba ambayo inadaiwa kufanyika
vitendo vya kutoa mimba. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.
========== ======== ========
JESHI la
polisi mkoani Kilimanjaro limefanikiwa kumnasa daktari mstaafu wa hospitali ya
rufaa ya Mawenzi,mkoani Kilimanjaro, Frances Shayo(56) akiwa katika harakati za
kuwatoa mimba wanawake wawili akiwemo Irene Musa(18) mwanafunzi wa shule ya
sekondari Nkwereko iliyoko Masama wilayani Hai.
Daktari huyo ambaye anatajwa kufanya vitendo hivyo mara kwa mara amekamatwa pamoja na watu wengine watano wakiwa katika nyumba ya mkazi wa Kata ya Ng’ambo aliyefahamika kwa jina moja na Minde.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema daktari huyo amekuwa akifanya shughuli hiyo kwa muda mrefu katika eneo hilo na mara nyingine amekuwa akifanya shughuli za kuwatairi watoto katika nyumba ya rafiki yake huyo.
Akizungumza na waandishi wa habari daktari Shayo amesema msichana huyo alifika katika nyumba hiyo akiwa na tatizo la kufunga kutokwa na damu hivyo alikuwa kwenye harakati za kutaka kumsaidia.
Kwa upande wake mama mzazi wa binti huyo,Rozi Urasa amesema alifika nyumbani kwa daktari huyo baada ya kushauliwa na baadhi ya ndugu zake kumpeleka kutoa ujauzito huo kutokana na kwamba huenda binti huyo akakosa kazi pindi atakapokuwa akitafuta kazi akiwa na ujauzito.
Daktari huyo ambaye anatajwa kufanya vitendo hivyo mara kwa mara amekamatwa pamoja na watu wengine watano wakiwa katika nyumba ya mkazi wa Kata ya Ng’ambo aliyefahamika kwa jina moja na Minde.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema daktari huyo amekuwa akifanya shughuli hiyo kwa muda mrefu katika eneo hilo na mara nyingine amekuwa akifanya shughuli za kuwatairi watoto katika nyumba ya rafiki yake huyo.
Akizungumza na waandishi wa habari daktari Shayo amesema msichana huyo alifika katika nyumba hiyo akiwa na tatizo la kufunga kutokwa na damu hivyo alikuwa kwenye harakati za kutaka kumsaidia.
Kwa upande wake mama mzazi wa binti huyo,Rozi Urasa amesema alifika nyumbani kwa daktari huyo baada ya kushauliwa na baadhi ya ndugu zake kumpeleka kutoa ujauzito huo kutokana na kwamba huenda binti huyo akakosa kazi pindi atakapokuwa akitafuta kazi akiwa na ujauzito.
PICHA ZAIDI BOFYA
HAPA


Ndio maana polisi wetu wana kuwa accused kwa excessive use of force; sasa hapo AK 47 wametinga nazo za kazi gani...unahitaji silaha nzito kiasi hicho kumkamata doctor?????
ReplyDeletePolisi watanzania bwana, kweshnei kabisa. Baada ya kwenda na mabunduki kumtafuta jambazi, mnaenda kutamfuta mtu ambaye hana silaha. Kwani anawalazimisha wanawake watoe mimba au wanaenda wenyewe.
ReplyDeleteMdau Kibaha
hili suala la POLISI kuvaa nguo za kawaida naona kama lipitiwe tena linachangia kiasi kikubwa cha ujambazi na kuuawa kwa raia wasio na hatia TANZANIA hatujafikia hayo kwanza
ReplyDelete