Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (wa tatu kutoka kushoto) akikata uteepe kuashiria uzinduzi rasmi wa zoezi la kugawa matrekta ya mkopo  kwa wakulima kutoka wilaya za mkoa wa dodoma, hafla hiyo ilifanyika leo kwenye ofisi za Kampuni ya NAM Ltd mjini Dodoma ambayo inakopesha matrekta hayo kwa wakulima, jumla ya matrekta matano yenye  thamani ya shilingi 175,000,000/-  yalikopeshwa kwa wakulimaleo hii.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi (kulia) akimkabidhi funguo ya trekta mkulima Kalanga Ngudong' wakai wa hafla ya kukabidhi kwa wakulima matrekta hayo ya mkopo yaliyotolewa na kampuni ya kusambaza matrekta ya NAM Ltd ya Mjini Dodoma, anayeshuhudia katikati ni mkurugenzi mtendaji wa NAM Ltd Bw. Aspenas Mwaranga, hafla hiyo ilifanyika leo mjini Dodoma.
Mkulima Kalanga Ngudong' kutoka kijiji cha Magungu Chamwino Dodoma akiwasha trekta lake alilokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma (hayupo pichani) baada ya mkulima huyo kupata mkopo wa trekta hilo kutoka kwa kampuni ya NAM Ltd ya mjini Dodoma iinayokopesha matrekta hayo (NAM Truck), hafla hiyo ya kukabidhi matrekta hayo ilifanyika leo hii kwenye viwanja vya kampuni ya NAM mjini Dodoma.  PICHA NA JERRY MWAKYOMA WA OFISI YA MKUU WA MKOA DODOMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...