Na Mary Gwera,Mahakama ya Tanzania
JUMLA ya Mashauri 188 yanatarajiwa kusikilizwa na kutolewa maamuzi katika kipindi cha mwezi Novemba na Disemba kufuatia vikao (sessions) vya Mahakama ya Rufani (T) vilivyoanza rasmi wiki hii katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza pamoja na Zanzibar ambapo kikao chake kitaanza rasmi tarehe 02.12.2013.
JUMLA ya Mashauri 188 yanatarajiwa kusikilizwa na kutolewa maamuzi katika kipindi cha mwezi Novemba na Disemba kufuatia vikao (sessions) vya Mahakama ya Rufani (T) vilivyoanza rasmi wiki hii katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza pamoja na Zanzibar ambapo kikao chake kitaanza rasmi tarehe 02.12.2013.
Hayo yamebainishwa na Kaimu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Zahra Maruma katika taarifa yake juu ya kufanyika kwa vikao hivyo vya Mahakama hiyo na kubainisha kuwa miongoni mwa Mashauri yatakayosikilizwa yanahusisha mashauri ya Rufaa za jinai, madai pamoja na maombi mbalimbali ya Rufaa hizo.
Mhe. Maruma aliongeza kuwa kwa upande wa Arusha jumla ya Rufaa 45 zitasikilizwa na kutolewa maamuzi, 35 zikiwa ni Rufaa jinai (criminal appeal) na kumi (10) maombi ya madai (civil application).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...