Waziri wa Maji na umwagiliaji,Profesa,Jumanne  Maghembe(kulia)akizungumza na Mkurugenzi wa Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi  nchini(GEPF)Daudi Msangi(kushoto)walipokutana kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma mara baada ya bunge kupitisha muswada wa marekebisho ya mfuko wa(GEPF),katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya mfuko huo Joyce Shaidi.
 Waziri wa Kazi Ajira na maendeleo ya Vijana,Gaudensia  Kabaka(kushto)akijadiliana jambo na Mbunge wa Kigoma mjini CCM,Peter Serukamba(kulia)nje ya ukumbi wa bunge mjini Dodoma,mara baada ya bunge kupitisha sheria ya marekebisho ya mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi nchini(GEPF)katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya kusimamia Mifuko ya hifadhi ya Jamii nchini,(SSRA)   Irene  Isaka
  Waziri wa Habari Vijana utamaduni na michezo,Dk.Fenella Mukangara,(kulia)akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex  Msama,  ambae pia ni  mjumbe wa Bodi ya Baraza la sanaa Taifa (BASATA)walipokutana nje ya ukumbi was Bunge mjini Dodoma,(katikati)ni Mbunge wa Peramiho,CCM,Jenista Mhagama.
 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,Jaji,Francins  Mtungi,(kulia)akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama(kushoto) Promotions,Alex Msama,walipokutana nje ya ukumbi wa bunge mjini Dodoma mara baada ya Rais Kikwete kulihutubia Bunge(katikati)ni Mbunge wa Jimbo la Peramiho,CCM,Jenista Mhagama.
 Katibu Mkuu wa CCM,Abdurahman Kinana(kulia)akisalimiana na Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka.katikati  ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama,Promotions,Alex Msama walipokutana kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Naona matukio ya Alex Msama akiwa bungeni yameibuka tena na yeye anapokea posho za vikao bungeni nini?

    ReplyDelete
  2. Hivi huyu Msama ni Mbunge wa Jimbo gani, maana kila tunapoambiwa matukio ya bungeni naye yumo, ama ndio 2015 maandalizi? au ofisi kahamishia bungeni, duh!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...