Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akizungumza na ujumbe wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na shirika hilo. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Dk. Peter Witterauf, anayefuata ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert, na Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo nchini Tanzania, Konrad Teichert. Viongozi wa Shirika hilo lenye Makao Makuu yake jijini Munich nchini Ujerumani walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation, Dk. Peter Witterauf. Kulia ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert. Viongozi wa Shirika hilo kutoka Makao Makuu, Kanda ya Afrika pamoja na Mwakilishi Mkazi wa shirika hilo nchini walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na shirika hilo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Dk. Peter Witterauf, wa pili kulia ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo nchini, Konrad Teichert na kulia ni Naibu Kamishina wa Polisi Makao Makuu, Tathimini na Ufuatiliaji, (DCP) Omar Rashid. Viongozi wa Shirika hilo lenye Makao Makuu yake jijini Munich nchini Ujerumani walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na Shirika hilo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...