Afisa Mazingira Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Japhet Kanizius, Akimkaribisha Mgeni Rasmi Bi. Magdalena Mtenga, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) kufungua rasmi warsha ya mafunzo kwa mafundi wa kuhudumia majokofu na viyoyozi kutoka Mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa. Mafunzo haya yanafanyika katika Hotel ya Mbeya Paradise Inn, Jijini Mbeya.
Sehemu ya washiriki kutoka Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Mgeni Rasmi, Bi. Magdalena Mtenga, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira).
Washiriki wa Warsha ya mafunzo kwa mafundi wa kuhudumia majokofu na viyoyozi kutoka Mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi Bi. Magdalena Mtenga Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais (Waliokaa - kwanza kushoto). Mafunzo haya yanafanyika katika Hotel ya Mbeya Paradise Inn, Jijini Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...