Nyumba ya moja mali ya Mzee Nampembe,Mkoani Lindi. imeteketea kwa moto jana Usiku na kupelekea baadhi ya mali zilizokuwemo ndani ya nyumba huyo kushindwa kuokolewa. Hali hiyo ilipekekea Wananchi wa eneo la jirani na nyumba hiyo kupiga mawe gari la zimamoto baada ya kuchelewa kufika eneo la Tukio kwa ajili ya kuzima moto huo.
Mmoja kati ya wakazi wa nyumba hiyo amepoteza fahamu toka jana baada ya kupatwa na Mshituko. Chanzo cha Moto imeelezwa kuwa ni Mshumaa baada ya kukosekana Umeme mjini Lindi usiku wa jana.
Picha na Abdulaziz Video, Lindi
Wasamalia waliokuwepo eneo la tukio wakisaidiana kumbeba mtu mmoja aliepoteza fahamu baada ya kutokea kwa tukio hilo.
Vilio vilitawala wakazi wa nyumba hiyo baada ya kutokea kwa tukio hilo.
Sehemu ya mali zilizookolewa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...