Picha ya pamoja kati ya mkuu wa wilaya chamwino Fatma Ally (wapili kushoto waliokaa) mwakilishi wa vodacom Salum mwalimu (kushoto waliokaa) pamoja na waandishi wa habari mkoa wa dodoma muda mfupi baada ya vodacom kukabidhi msaada wa computer 3 na router ya kuunganisha computer na mtandao kwa chama cha waandishi wa habari mkoa wa dodoma Leo,msaada hug unathamani ya zaidi ya million 5.
Mkuu wa wilaya chamwino Fatma Ally kushoto akimkabidhi mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa dodoma CPC Joyce kasiki kulia computer zilizotolewa na vodacom kama msaada kwa chama waandishi wa habari mkoa wa dodoma ili kusaidia shuguli zao za uandishi wa habari, anayeshuhudia katikati ni mwakilishi wa vodacom Salum mwalimu.Kushoto.
Mkuu wa wilaya chamwino Fatma Ally akisisitiza waandishi wa habari wa dodoma kuboresha utendaji kazi, kufanya tafiti za mtandaoni na kutoa habari na taarifa zenye ubora wa hali ya juu kutumia msaada wa computer 3 na rooter ya kuunganisha mtandao vilivyotolewa na Vodacom kama msaada kwa waandishi hao, hafla yamakabidhiano ilifanyika ofisi za waandishi wa habari mjini dodoma Leo.Msaada.
Mwakilishi wa vodacom Salum mwalimu akielezea azma ya vodacom kusaidia vyama vya waandishi wa habari vya mikoa ili kusaidia kunyanyia ubora wa shughuli za uandishi wa habari hapa nchini, jumla ya computer 3 na rooter ya kuunganisha mtandao vyenye shaman ya zaidi ya milioni 5 vimetolewa na vodacom vodacom kama msaada kwa waandishi wa habari mkoa wa dodoma mapema Leo. (PICHA NA JEREMIA MWAKYOMA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...