Meneja wa benki ya Azania tawi la Moshi Hajira Mmbande(mwenye suti
nyeusi) akimkabidhi cheti mmoja wa wafanyakazi katika benki hiyo
Tumsifu Invocarith ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya tawi hilo.
Meneja wa benki ya Azania tawi la Moshi Hajira Mmbande(mwenye suti
nyeusi) akimkabidhi cheti mmoja wa wafanyakazi katika benki hiyo
happness msengi ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya tawi hilo.
Wafanyakazi wa benki ya Azania tawi la Moshi wakiwa katika picha ya
pamoja na vyeti vyao walivyokabidhiwa kama sehemu ya mafanikio ya tawi
hilo.
Wafanyakazi wa benki ya Azania tawi la Moshi wakiwa katika picha ya
pamoja na zawadi mbalimbali walizokabidhiwa baada ya kufanikisha tawi
hilo kuwa miongoni mwa matawi yaliyopata mafanikio katika kipindi cha
muda mfupi.
Wafanyakazi wa benki ya Azania tawi la Moshi wakigonga Cheers
kufurahia mafanikio katika tawi hilo.
Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.
MENEJA wa benki ya Azania tawi la Moshi,Hajira Mmbande amepongeza
uongozi wa benki hiyo ambao pia ni wakurugenzi kwa kuwezesha tawi hilo
kuwa miongoni mwa matawi yaliyopata mafanikio ndani ya kipindi kifupi.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha
mwaka 2014 iliyoenda sanjari na pongezi kwa wafanyakazi wa tawi hilo
Bi Mmbande aliwapongeza wakurugenzi hao ambao ni mifuko ya hifadhi ya
jamii, NSSF,PPF,PSPF,LAPF na Benki ya Maendeleo ya Afrika
Mashariki(EADB) pamoja na wanahisa wengine.
Aliipongeza pia Kurugenzi ya Azania bank chini ya uongozi wa Bw
Charles Singili ,watumishi wote wa banki ya Azania hususani wale wa
tawi la Moshi pamoja na wateja wote wa banki ya Azania kwa ushirikiano
wao wa pamoja ulioowezesha kupatikana kwa mafanikio hayo ndani ya
kipindi kifupi toka kufunguliwa kwa tawi hilo mjini Moshi .
Bi Mmbande alitoa rai kwa kila mdau wa benki ya Azania kuongeza ari
,kasi na ushirikiano katika mwaka huu mpya wa 2014 ili kuifanya benki
ya Azania iwe bora zaidi na kufikisha huduma kwa kila mtanzania kama
ambavyo inavyojitangaza kwa watanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...