Na; Inspekta Lucas Mboje, Jeshi la Magereza
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja amekemea vikali tabia ya baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wenye tabia ya kutofuata Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo katika utendaji wao wa kazi za kila siku hivyo ameonya kuwa yeyote atakayekwenda kinyume hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake bila kujali cheo au wadhifa alionao.
Kamishna Jenerali John Minja ameyasema hayo juzi wakati wa Baraza la Kufunga Mwaka 2013 na kuukaribisha Mwaka 2014 lililowahusisha baadhi ya Maafisa na Askari kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, D'Salaam, Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani(KMKGM) pamoja na Magereza Mkoa wa D'Salaam.
Aidha, amewataka Maofisa, Askari na Watumishi wote kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea bali wawe wabunifu kwa kutumia raslimali zilizopo kwenye maeneo yao ya kazi ili kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...