Watu 13  wanasemekana wamepoteza maisha baada ya  gari ya abiria aina ya Noah walilokuwamo kupata ajali kwa kugongwa na lori mkoani Singida hivi punde. Habari zinasema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo wa kasi na dereva kushindwa kumiliki lori hilo na kujikuta likipinduka  na kusababisha maafa hayo. Waliopoteza maisha ni pamoja na  dereva na msaidizi wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Wataalamu wameshasema, Noah haifai kuwa gari ya abiria, lakini hapa TZ tunakuwa wakahidi!! Au ni katika population control??!! Kuna wageni wakitoka nje huwa hawapandi kabisa hizi Noah tulizozihalarisha kubeba abiria na mizigo!!

    Sina cha kuongezea, ila kusubiri jinsi waTZ wanavyopunguzwa kwa uzembe wa hali ya juu!!

    ReplyDelete
  2. Mbona Bongo kuna ajali kama hizi za kutisha kweli. Agalia hilo gari lilivyoteketea utafikiri lilikuwa limejengwa kwa vigai na majaribosi.

    ReplyDelete
  3. Ukipakia watu kwenye boksi, halafu kwenye highway unategemea nini?? Juzi juzi tu huko moro au dom Noah ilifyeka wote hakuna hata wa kusimulia kilichotokea!! Nafikiri abiria waweke mgomo wa kuzipanda Noah!!

    ReplyDelete
  4. Pole wahanga wote wa ajali, sala zangu ziende kwa majeruhi wote wapate nafuu mapema, na marehemu wote namwomba mwenyezi mungu awalaze roho zao mahali pema peponi, amen.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...