JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
    JESHI LA POLISI TANZANIA

               Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME ametoa tahadhari kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma kuwa na tahadhari katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha maeneno mbalimbali.

Ametoa thahadhari hiyo baada ya kutokea tukio la PHILIPO SUNGURA, Miaka 55, Mgogo Mkazi wa Kijiji cha Mpinga Kata ya Kigwe Wilayani Bahi kufa maji wakati akijaribu kuvuka mto Mpinga ambao ni wa msimu. Tukio hilo lilitokea tarehe 24.01.2014 majira ya saa 18:45 jioni wakati akijaribu kuvuka mto huo huku maji yakiwa ni mengi.

Kamanda Misime ameeleza imembidi kutoa tahadhari hiyo kwani kumbukumbu zinaonyesha watu wengi hupoteza maisha inapofika msimu wa mvua wakiwemo watoto wanaokwenda kuoga na kuchota maji katika mabwawa, mito ya msimu na madimbwi yaliyotuama maji kwa kunasa kwenye tope na kupoteza maisha.

Mfano anaeleza tangu mvua za msimu zilipoanza mwaka huu 2014 watu wanne (4) wameshapoteza maisha.

Amewaomba Viongozi wa Mitaa, Vitongoji, Vijiji, Kata, Tarafa na waalimu mashuleni kuwaeleimisha wananchi na wanafunzi ili kuepukana na matukio hayo.
         

                           [DAVID A. MISIME - SACP]

                        KAMANDA WA POLISI MKOA WA DODOMA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ktk miaka yote ni leo tu ndio nimefarijika kuona Tangazo lililojaa Uzalendo na Uwajibikaji...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...