Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. George D. Yambesi akifungua mkutano wa wadau kuhusu Mikataba ya Utendaji Kazi katika Taasisi za Umma katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Mkutano huo uliandaliwa mahsusi ili wadau waweze kufahamu mambo muhimu juu ya Mfumo wa Mikataba ya Utendaji Kazi hususan chimbuko, maana na faida zake, mambo ya msingi yatakayofanikisha utekelezaji wa mfumo huo, fomu ya mkataba wa utendaji kazi na vipengele vyake, vigezo vya upimaji wa utendaji kazi wa taasisi, wahusika wa mikataba na utaratibu wake; utaratibu wa kutoa taarifa za mikataba ya utendaji kazi, utaratibu wa kutathmini mikataba ya utendaji kazi; utaratibu wa kushindanisha Taasisi za Umma; na Taasisi zinazopendekezwa kuingia katika Mikataba ya Utendaji Kazi . Sambamba na hilo wadau walipata fursa ya kutoa maoni, ushauri na mapendekezo juu ya mfumo wa Mikataba ya Utendaji Kazi, na namna bora ya kuitekeleza katika Taasisi za Umma. Wadau walioshiriki mkutano huo ni pamoja na watendaji na watendaji wakuu wastaafu katika Taasisi za Umma wakiwemo Makatibu Wakuu wastaafu, watendaji wakuu wa Asasi za Kiraia (AZAKI), wanataaluma kutoka vyuo vya Elimu ya juu, wawakilishi kutoka katika sekta binafsi na Washauri waelekezi Wanaojitegemea.
Sehemu ya baadhi ya wadau walioalikwa katika Mkutano kuhusu Mikataba ya Utendaji Kazi katika Taasisi za Umma wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. George D. Yambesi (hayupo pichani).
Wadau walioshiriki mkutano kuhusu Mikataba ya Utendaji Kazi katika Taasisi za Umma wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. George D. Yambesi (wa sita kutoka kulia mstari wa mbele), kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu Bw. HAB Mkwizu na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri Kazi Bw. Mick Kiliba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...