Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akiongea katika mkutano a Mazungumzo ya usuluhishi wa mgogoro wa mpaka baina ya Tanzania na Malawi kwenye Ziwa Nyasa yameanza leo Jijini Maputo, Msumbiji kwa kuzikutanisha pande zote mbili za mgogoro huo. 
Mazungumzo hayo yaliyopo chini ya Jopo la Usuluhishi linaloongozwa na Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joachim Chissano akisaidiwa na Mhe. Thabo Mbeki Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini na Mhe. Festus Mogae Rais Mstaafu wa Botswana yaliwapa nafasi pande zote mbili kutoa tamko rasmi kabla ya usuluhishi kuanza. 
Ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo hayo yanoyotarajia kuchukua siku mbili umeongozwa na Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Anna K. Tibaijuka, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Frederick M. Werema, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dr. David S. Mayunga, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na wataalamu wengine kutoka taasisi mbalimbali za Serikali.
Aidha ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo haya umejumuisha Wabunge wawili kutoka Kanda ya Ziwa ambao ni Mhe. Kapt. John Komba na Mhe. Deo Filikunjombe.
Hapa chini ni tamko rasmi la Tanzania Kama lilivyowasilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Well constructed arguments.. I hope we will hear what Malawi will have to say too

    ReplyDelete
  2. Sipati picha kuwa watu wa mbambabay wakitaka kitoweo au kuogelea ziwani waende Blantyre kuchukua viza!

    ReplyDelete
  3. your excellence minister of foreign affairs....we thank you for your logical presentation

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...