Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Mkoko wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi kumgombea Ubunge jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete ambapo wananchi hao walielezwa kitendo cha kuzuiwa kupiga kura ni sawa na ubakaji wa Demokrasia na CCM itakula sambamba na wabakaji wa Demokrasia.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye pia ndiye Mratibu wa kampeni za mgombea wa CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete akionyesha kadi Chadema  iliyorudishwa na Ndugu Subira Mrisho ambaye alikuwa mhamasishaji wa Chadema katika kijiji cha Mkoko,pia katika kata ya Msata Katibu Kata wa Chadema amerejea CCM anaitwa Mrisho Issa pamoja na mwananchama mwingine anayejulikana Kassim Msakamali wamerejea CCM
 Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Shaibu Akwilombe akihutubia wakazi wa kijiji cha Mkoko kwenye mkutano wa kumnadi mgombea wa CCM Ndugu Ridhwani Kikwete.
 Mtela Mwampamba akihutubia wakazi wa kijiji cha Mkoko na kuwasihi wananchi hao kutambua mahusiano ya Tanzania na Chama Cha Mapinduzi.
 Diwani wa Kata ya Msata akiwahutubia wananchi wa kiji cha Mkoko wakati wa kumtano wa kampeni wa kumnadi mgombea wa CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...