NMB imezindua  rasmi tawi la jipya la Buzuruga mkoani Mwanza, likiwa ni tawi la tisa kuzinduliwa katika mkoa wa huo, huku NMB ikiendelea kuwa ndio benki yenye matawi mengi zaidi Tanzania.
Akizungumza katika sherehe ya ufunguzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mh. Baraka Konisaga ameipongeza benki ya NMB kwa hatua nyingine iliyopiga kwa  kusogeza zaidi huduma kwa wateja  na kuitaka iendelee kuwa kinara wa huduma za kibenki nchini. 
Aliwahamasisha wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi waitumie fursa ya kuwepo kwa tawi la NMB Buzuruga kukidhi mahitaji yao ya kibenki. Vilevile, aliwasihi wananchi waache kuweka fedha kwenye chaga za vitanda na badala yake watumie njia salama ya kuweka fedha benki.
 “Ni matumaini yangu kuwa uwepo wa tawi hili la Buzuruga ni neema kubwa kwa wakazi wa Mabatini, Buzuruga, Nyakato, Igoma, Kishili, Buswelu na hadi Kisesa hasa wafanyabiashara katika hizi mashine za mpunga kwani kesi za watu kuporwa fedha majumbani au maofisini zitapungua badala yake ongezeko la wateja wanaofungua akaunti ndio itakua habari ya eneo hili” alisema Konisaga.
 Kwa upande wake, Bw. Straton Chilongola, ambae ni Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, alisema “Tangu kuanzishwa kwa tawi hili tumeshuhudia wakazi wengi wa wakija kufungua akaunti na kutumia huduma za benki hii. Hii ni uthibitisho kuwa wakazi hawa walikua na kiu ya kupata huduma za kibenki karibu kariba na milangoni kwao. Lakini pia tutaendelea kubuni mbinu mbalimbali zitakozotuwezesha kuwafikia wateja wetu karibu zaidi ili kuondoa msongamano kwenye matawi na pia kuokoa muda wa wateja ili waweze kutumia muda wao kwa shughuli endelevu.” 
Tawi hili la Buzuruga, linatoa huduma zote za kibenki, ikiwa ni pamoja na huduma ya mikopo ya aina mbali mbali bila kusahau mikopo ya Kilimo. Tawi hili litakua wazi kila Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa mbili na nusu asubuhi hadi saa kumi na jioni ( 2:30 asubuhi  - 10:00 jioni) na Jumamosi kuanzia saa mbili na nusu asubuhi hadi saa sita na nusu mchana (2:30 asubuhi - 6:30 mchana), Jumapili na siku za Sikukuu hakutakuwa na huduma ndani ya tawi hili. NMB daima benki yako!
 Kikundi cha ngoma cha Bujora kikitumbuiza katika hafla ya uzinduzi huo.
Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya wa Nyamagana, Bw. Baraka Konisaga akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la NMB Buzuruga. wakishuhidia uzinduzi huo kutoka kushoto ni Naibu Meya Jiji Mwanza mhe. John Minja, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza  Bw. Halifa H. Hida na kutoka kulia ni Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Bw. Straton Chilongola, Meneja Tawi la NMB Buzuruga, Gadiel Sawe na Meneja Mawasiliano wa NMB , Josephine Kulwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...