Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi. Theresia Mmbado akifunga mafunzo ya siku 3 ya matumizi ya Fomu za OMR kwa walimu wakuu 254 wa shule za Msingi za mkoa wa Dar es salaam yaliyofanyika katika shule ya Sekondari Shaaban Robert.
Afisa Elimu wa mkoa wa Dar es salaam Bw. Raymond Mapunda akitoa ufafanuzi kwa walimu wakuu wa shule za Msingi za mkoa wa Dar es Salaam kuhusu namna mkoa ulivyojipanga kutatua changamoto za elimu.
Baadhi ya Walimu wakuu wa shule za Msingi jijini Dar es salaam wakifuatilia michango mbalimbali iliyokuwa ikiwasilishwa kuhusu maboresho ya matumizi ya mfumo wa OMR.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
Matumizi ya mfumo mpya wa kufanya mitihani kwa kutumia karatasi maalum za OMR (Optical Mark Reader) na usahihishaji wa mitihani hiyo kwa njia ya kompyuta umeonyesha mafanikio jjini Dar es salaam mara baada ya vitendo vya udanganyifu na wizi wa mitihani ya shule ya msingi kudhibitiwa.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi. Theresia Mmbado ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es salaam wakati akifunga mafunzo ya siku 3 ya matumizi ya Fomu za OMR kwa walimu wakuu 254 wa shule za Msingi za mkoa wa Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...