Na Greyson Mwase, Ujerumani
Tanzania inatarajiwa kuondoka kwenye kundi la nchi masikini na kuhamia kwenye kundi la nchi zenye kipato cha kati ifikapo mwaka 2025. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alipokuwa akifungua kongamano linaloendelea huko Berlin nchini Ujerumani kama njia mojawapo ya kuadhimisha jubilee ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kongamano hilo linakutanisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabalozi, wataalamu na wafanyabiashara mbalimbali ambapo Profesa Muhongo alipata nafasi ya kuwasilisha mada kuhusiana na fursa zilizopo katika sekta ya gesi, mafuta ikiwa ni pamoja na madini.
Profesa Muhongo alisema ili nchi ya Tanzania iweze kupiga hatua kimaendeleo inahitaji uwekezaji mkubwa kwenye nishati ambayo ndiyo yenye mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi.
Akielezea juhudi za serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa na maisha bora, Profesa Muhongo alisema kuwa serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza juhudi za kupeleka umeme kwenye vijiji vyote kwa awamu tofauti tofauti.
“ Hatuwezi kusema kuwa nchi imeendelea wakati wananchi wa vijijini hawana umeme, na katika kutambua hilo serikali imeweka nguvu nyingi kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inapatikana vijijini na kuchochea maendeleo.” Alisisisitiza Profesa Muhongo.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...