Wachezaji wa Atlético Madrid wakishangilia ushindi wao dhidi ya Barcelona jana.   Baada ya kuisambaratisha Real Madrid katika uwanja wao wa Santiago Bernabeu na kunyakua kombe la Copa del Rey (Kombe la Mfalme) mwaka uliopita,  Atlético Madrid jana wamefanya maajabu mengine baada ya kunyakua ubingwa wa La Liga mkononi mwa Barcelona ya kina Messi kwa kutoka nao droo ya 1-1. 
Ni ubingwa wao wa kwanza katika miaka 18. Kifuatacho ni kucheza fainali za  mabingwa wa Ulaya baada ya miaka 40! Mambo hayo ya Diego Simeone  na timu yake hiyo si ya kawaida. Hata mashabiki wa Barca walilitambua hilo baada ya filimbi ya mwisho ambapo waliinuka na kuwashangilia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 19, 2014

    Huyo anaitwa Diego Simeone aka Cholo...Bado na ubingwa!

    Sasa sijui waspain kwanini wanamuita cholo?! Sijui cholo huyu huyu wa kwetu Zenji?!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...