Marehemu Adam Kuambiana enzi za uhai wake.

MWIGIZAJI na Muongozaji filamu maarufu Bongo, Adam Kuambiana amefariki dunia wakati akipelekwa hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam kwa matibabu alfajiri ya leo. 

Habari zinasema Marehemu alianguka chooni akiwa location katika hoteli ya Silver Rado iliyopo Sinza kwa Remmy, Dar es salaam. 
Kabla ya mauti kumfika, Adam alikuwa akilalamika kuwa anasumbuliwa na tumbo.
Globu ya Jamii inaungana na familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na wadau wote wa Bongo Movie katika kuomboleza kifo cha nyota huyu wa filamu.
Mola aiweke roho ya marehemu
mahala pema Peponi
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2014

    jamani hili tumbo la siku hizi mpaka linatuletea mauti ni nini?Amina ngaluma nae alikuwa analalamika tumbo tumbo mpaka mauti imemchukua,Mungu tunusuru.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 18, 2014

    Nimesikitika sana na kikubwa zaidi ni ile kupuuzia na kupotezea magonjwa yanapoanza. Ni vema tuwe tunaenda kuchekiwa mara kwa mara haswa chochote kinachohusu damu, iwe kutapika, kukohoa, hata choo. Nimeshaumwa na nyoka nikapona kwa rehema ya Mungu sasa nikiona na mwingine amepatwa na janga hili tuwe macho kwa kweli. Alikuwa na kipaji cha pekee

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...