Kanali Dr. Edward Massala kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania ( JWTZ) akifuatilia majumuisho ya Mkutano wa Tatu wa Maadalizi ( Prep CoM) ya mapitio ya Mkataba wa Kimataifa wa Uzuiaji wa Usambaaji Holela wa Silaya za Nyukilia ( NPT) Mkutano huo wa maandalizi ulifanyikak wa wiki mbili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Ingawa wajumbe kutoka nchi 149 kati ya 189 ambazo ni wanachama wa NPT hawakutoka na makubaliano ya pamoja kuhusu mapendekezo na mpango wa utekelezaji vinavyokusudiwa kuwasilishwa kwenye mkutano huo wamapitio utakaofanyika mwaka 2015. jambo la msingi ambalo kila nchi inalikubali ni kwamba hakuna nchi au shirika litakaloweza kukabiliana na madhara ya mlipuko wa silaha za nyukilia na kwamba jambo la muhimu ni kuondokana kabisa na silaha hizo ili dunia iwe mahali salama. Nyuma ya Kanali Massalla ni Bw. Abdalla Khamis, Afisa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa
Na Mwandishi Maalum
Mkutano wa Tatu wa maandalizi ( Prep Com) ya mkutano utakaofanyia mapitio ya Mkataba
wa Kimataifa Unaozuia Usambaaji Holela wa Silaha za Nyukilia ( NPT) umemalizika
mwishoni mwa wiki iliyopita, huku wanachama wakitoka bila ya kuwa na makubaliano ya
pamoja kuhusu mapendekezo na mpango wa utelelezaji yatakayowasilishwa katika mkutano
huo wa mapitio unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015.
Licha ya kwamba nchi hizo hazikutoka na makubaliano ya pamoja, jambo la msingi na ambalo
linakubalika na wote ni kwamba hakuna nchi au shirika la kimataifa linatakaloweza kukabiliana
na madhara ya mlipuko wa silaha za nyukilia iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya.
Na kwa sababu hiyo nchi 136 zilizochangia hoja ya madhara ya silaha za nyukilia kwa
binadamu zilisisitiza kuwa njia pekee ya kumwepusha mwanadamu na madhara hayo ni
kuondokana au kuachana kabisa na silaha za hizo.
Hata hivyo, nchi zinazomiliki silaha za nyukilia ambazo ni Ufaransa, Marekani, Uingereza,
China na Urusi, licha ya kutambua madhara ya silaha hizo, zenyewe zimependekeza kuwa
upunguzaji wa silaha hizo, ufanyike hatua kwa hatua.
Akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa mkutano huo uliofanyika kwa wiki
mbili kuanzia April 28 hadi Mei Tisa, Mwenyekiti wa mkutano huo wa Tatu Mwakilishi wa
Kudumu wa Peru katika Umoja wa Mataifa, Balozi Enrique Roman – Morey alieleza kwamba
kutofikiwa kwa makubaliano ya pamoja kuhusu mapendekezo na mpango wa utekelezaji
hakukutokana na kutokuwepo wa utashi wa kisiasa baina ya wajumbe bali ni ufinyu wa muda
zaidi wa majadiliano.
Kwa mujibu wa Balozi Morey nchi 149 kati ya 189 ambazo ni wanachama wa NPT
walihudhuria mkutano huo. Na kwamba nchi tano zinazomiliki silaha za nyukilia yaani
Marekani, Urusi, Uchina, Ufaransa na Marekani, ziliwasilisha taariza zao zinazofanana kuhusu
mchakato unaoendelea wa kupunguza malimbikizo ya silaha hizo.
Mwenye kiti huyo wa Prep Com alibainsha kwamba nchi wa wanachama wa NPT walijadili
vipengele muhimu vinayounda NPT ambavyo ni uzuiaji wa usambaaji holela wa silaha za
nyukilia, upokonyaji wa silaha za nyukilia, matumizi salama ya nishati ya nyukilia, madhara
ya nyukilia kwa mwanadamu na Uanzishwaji wa Ukanda huru dhidi ya silaha za nyukilia na
silaha zingine za maangamizi katika eneo la Mashariki ya kati.
Aidha Balozi alieleza pia kwamba jambo jingine lililojadiliwa kwa mapana na wanachama
wa NPT ni kuhusu haja na umuhimu wa mataifa kuridhia mkataba wa kimataifa unaozuia
majaribio ya silaha za nyukilia (CTBT). Hadi sasa ni nchi 162 tu ndizo zilizoridhia mkataba
huo.
Jambo la muhimu ambalo Mwenyekiti wa PrepCom anasema lilionekana dhahiri katika
mkutano huo ni kuwa nchi zote zilizoshirikia mkutano huo wa maandalizi, zimeonyesha
uwajibikaji katika kuhakikisha kuwa Dunia inaondoka na inakuwa huru dhidi ya silaha za
nyukilia.
Mapendekezo na mpango wa utekelezaji uliopitishwa mwishoni mwa mkutano huo,
utawasilishwa na Mwenyekiti wakati wa mkutano wa mapitio ya NPT utakofanyika mwezi Mei
mwaka 2015.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutao huo uliongozwa na Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa
Tanzania katika Umoja wa mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akiwamo mtaalamu kutoka
Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Kanali Dr. Edward Massala.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...