Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Mh Dkt. Seif Rashid na Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mh. Dkt. Juma Duni wakifuatilia kwa Makini Mkutano wa 67 wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHA) uliofunguliwa leo Jijini Geneva,Uswiss na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Dr Margareth Chang.Mada kuu ya Mkutano wa mwaka huu ni "The link between climate and health" yaani Uhusiano kati ya mabadiliko ya tabia nchi na Afya.Vile vile pamoja na Mada nyingi zitakazozungumziwa katika Mkutano huu wa siku Sita, Mke wa Rais wa Zambia Dr Christine Kaseba-Sata ambaye ni Balozi maalum wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kuhusu ukatili wa kijinsia na Bi Melinda Gates,Mwenyekiti mwenza wa Bill&Melinda Gates Foundation wata wasilisha mada kuhusu maeneo hayo.
Baadhi ya Wajumbe wa Tanzania wakiandaa mada zitakazo wasilishwa katika Mkutano huu uliofunguliwa leo Jijini Geneva,Uswiss.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 19, 2014

    ile world health organisation(WHO) imekua world health "Associatio"?(WHA)

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...