Na John Gagarini, Kibaha 

MLINZI Bakari Mape (70) mkazi wa Mlandizi wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani ameuwawa kwa kunyongwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi.

Watu hao ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja walimwua mlinzi huyo kwa kumvunja shingo kisha kuiba kwenye duka ambalo mlinzi huyo alikuwa akililinda.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 14 mwaka huu majira ya saa 8 usiku eneo la sokoni Mlandizi wilayani hapa.

Kamanda Matei alisema kuwa watu hao baada ya kumwua marehemu ambaye alikuwa akilinda duka la Conrad Masawe (53) mkazi wa Mtongani Mlandizi, waliiba kiasi cha shilingi milioni 5.2.

"Walipomwua walingoa bati kisha kuingia ndani na kuiba fedha hizo na kutoweka kusikofahamika huku wakimwacha marehemu hapo," alisema Kamanda Matei.

Alisema kuwa kutokana na tukio hilo wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Omary Rajabu kuhusiana na suala hilo.

"Mwili wa marehemu ulikabidhiw andugu kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi wa daktari na tutawasaka watu walihusika na tukio hilo ili mkondo wa sheria uweze kuchukua hatua kwani kitendo hicho ni ukatili ndani ya jamii," alisema Kamanda Matei.

Aidha aliwataka wafanyabiashara waajiri watu weny umri wa kati ili waweze kukabiliana na matukio kama hayo na kuacha kuajiri watu wenye umri mkubwa sana kwani ni vigumu kukabiliana na matukio kama hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2014

    Kamanda.....umri huo yapaswa awe anapokea pensheni kila mwezi iliaweze kujikimu maisha lakini kwakua hatuna utaratibu huo, marehemu aliamua kujituma japo kwa umri wake huo, wapo wengi sana ambao si kwa kupenda wapo ktk ajira zisizo rasmi hivyo suala la kuwashauri waajiri watazame vijana tu si ushauri sahihi kwa mtazamo wangu.Hili la kuwapa fedha za kujikimu wazee lawezekana kwakua idadi yao kwa sasa si kubwa nchini, hii ni kwa mujibu wa takwimu. ....R..I..P

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...