Fainali za Kombe la Dunia ni uwanja mpana. Ni mahali ambapo vipaji na
vipaji vya wanasoka duniani huonekana. Madalali wa kuvumbua na kununua
wachezaji [scouts] hufurika kwenye mashindano kama haya wakijua wazi
kabisa kwamba pale ndipo watakapoona “lulu” kwa ajili ya vilabu vyao.
Kwa maana hiyo kuna kila aina ya harakati za kimichezo na kuonyesha na
kuonyeshana vipaji. Hii sio kumaanisha kwamba wachezaji wote mahiri hapa
duniani walicheza katika fainali za Kombe la Dunia.La.
Wapo wasakata
kabumbu kadhaa ambao hawakuwahi kugusa fainali hizi.Mfano ni George
Opong Weah na watu kama kina George West nk.
Lakini wakati wengine wakionyesha vipaji ili wang’amuliwe na
kubadilisha maisha yao ya kisoka,wapo wale ambao wanashuka dimbani
tayari wakiwa na majina [superstars] na ambao dunia tayari inakuwa
ikiwaangalia kwa makini kutaka kujua na kuona kile watakachokifanya.
Kila timu huwa na mchezaji ambaye hutizamwa zaidi. Kwa umombo unaweza
kumuita Key Player. Kila timu,kwa kupenda au kutopenda,huwa ina star
player. Hii haimanishi kwamba katika timu hakuna wachezaji wengine wenye
majina au wanaoweza pia kuwa stars.La. Ni sheria ya mmoja mmoja
inayozingatiwa hapa.
Kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali wa soka,wachezaji hawa 32 [mmoja
kutoka katika kila timu inayoshiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka
huu] ndio watarajiwa kuchomoza zaidi huko Brazil. Mpangilio huu hapa ni
kutokana na makundi ya FIFA World Cup 2014.
NB: Orodha hii inaweza kubadilika kwani imeandikwa kabla timu
zote hazijathibitisha wachezaji wake 23 iliyowachagua mwisho. Wengine
wanaweza kuumia katika siku hizi za mwisho na hivyo kutokwenda
Brazil.Zingatia.
Neymar-Brazil.
Hakuna ubishi kwamba Neymar anayechezea
soka la kulipwa Barcelona nchini Spain ndio gumzo kubwa kwa timu ya
Brazil. Anatarajiwa kuongoza mashambulizi ya The Kings Of Samba[Brazil]
Oribe Peralta-Mexico
Ingawa wachezaji wengine wa Mexico kama Chicharito na Giovani dos
Santos wanatajwa kama ma-star,Oribe Peralta ambaye anacheza katika ligi
ya nyumbani katika club ya Santos Laguna, ndiye anaaminika hivi sasa
kuwa star zaidi
Luka Modric-Croatia
Hakuna shaka kwamba Luka Modric ndiye mchezaji star zaidi hivi sasa
katika timu ya Croatia. Kiungo huyu ambaye hivi sasa anachezea timu ya
Real Madrid nchini Spain ameonekana wazi kuwa tegemeo sio tu katika club
bali nchi yake Croatia.
Charles Itandje-Cameroon
Ingawa ungetegemea mchezaji kama Samuel
E’too kuendelea kuwa star na tegemeo zaidi katika timu ya Cameroon,
golikipa Charles Itandje ndio tegemeo na ambaye wengi watapenda kumuona
akiokoa mikwaji. Charles ambaye anachezea timu ya Konyaspor nchini
Uturuki[kwa mkopo kutoka PAOK FC ya Ugiriki] aling’ara vilivyo katika
mchezo dhidi ya Tunisia wakati wa kuwania nafasi ya kwenda Brazil.Google
utaona alichofanya.
Diego Costa-Spain
Ingawa bado kuna utata kuhusu hali yake
na kama atakuwa fit kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia huko
Brazil,Diego Costa mshambuliaji mahiri wa timu ya Atletico Madrid
anatarajiwa kuwa nyota wa Spain. Lakini pia huenda akawa ndiye mchezaji
atakayezomewa zaidi huko Brazil kwani Diego ni mzaliwa wa Brazil na
angeweza kabisa kuchezea Brazil mwaka huu kama asingeamua kuchezea
Spain[pia ni raia wa Spain].Wabrazil hawajaipenda hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...