Baadhi ya Viongozi wa Idara za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wanaohudhuria kikao
cha kuandaa Mpango Kazi na Mpango wa Manunuzi wa Wizara hiyo katika Chuo cha Kanda
cha Uhamiaji mjini Moshi, (toka kulia) Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza,
Gaston Sanga, Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi, Clodwig Mtweve, Kamishna
wa Urekebishaji wa Jeshi la Magereza, Deonice Chamulesile na Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la
Polisi, Juma Mohamed.
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (aliyevaa tai) wakiwa katika Kikao cha kuandaa Mpango Kazi na Mpango wa Manunuzi kwa mwaka wa fedha 2014/15 kinachofanyika katika Chuo cha Kanda cha Uhamiaji mjini Moshi. Aliyesimama ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Manunuzi wa Wizara hiyo, Manyama Mapesi. Kikao hicho kinawajumuisha Watendaji Wakuu wa Idara za Wizara, Maafisa Bajeti pamoja na Maafisa Manunuzi.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...