Germany ndio mabingwa wa kombe la Dunia  2014 FIFA World Cup, wakinyakua kombe kwa mara ya nne katika historia yao baada ya kuwashinda  Argentina 1-0 kwa bao la muda wa nyoingeza la  Mario Gotze (pichani juu kushoto) katika uwanja wa Maracana huko Rio de Janeiro.

Mchezaji huyo aliyeingia kama mchezaji wa akiba aliweza kuua uwezekano wa kupigiana penati kwa bao lake la uamuzi baada ya timu hizo kutoka suluhu hadi mapumziko katika mchezo uliojaa kila aina ya msisimko. Bao lake hilo liliwamaliza kabisa Argentina ambao walishindwa kujibu mapigo, na Germany wakaongeza nyota ingine katika historia yao kufuatia ubingwa wao wa mwaka 1954, 1974 na 1990.

Wananchi wa Bagamoyo wakifuatilia mchezo wa fainali za kombe la Dunia usiku wa kuamkia leo ambapo Germany ilifanikiwa kunyakua kombe hilo dhidi ya Argentina ya kina Messi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 14, 2014

    Hongera Ujerumani kwa kulitwaa kombe. Mwaka 2018 je kutakuwa angalau na timu ya Afrika Mashariki?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 14, 2014

    Walistahili kwanza wamecheza nusu fainali mbili na fainali mbili ndani ya miaka 12 pili wana kocha ambaye wamekaa naye nafkiri zaidi ya miaka 10 makocha wengi hawadumu kukaa na tim za taifa miaka yote tatu wanamchanganyiko wa wachezaji wana asili ya mataifa tofauti wameachana na zambi ya ubaguzi wa rangi na dini hongereni sana

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 14, 2014

    Wananchi wa Bagamoyo katika hili eneo hapo wanahitaji ukumbi bora zaidi wa kuangalia mpira..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...