Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Joyce Mapunjo akizungumza na moja ya chombo cha habari wakati wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini ambaye ni Msemaji wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Vedastina Justinian akimsikilia mwananchi aliyetembelea banda la wizara hiyo kwenye maadhimisho ya wiki ya Utumishi ya Umma yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.Picha na Hussein Makame-MAELEZO.
============  =========
Hussein Makame-MAELEZO.

WAKATI Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki walipotia saini Mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1999, kila upande ulilenga maslahi ya kiuchumi na maendeleo kwa nchi na wananchi wake katika nyanja mbalimbali. Lakini ni ukweli ulio wazi kwamba mafanikio ya nchi katika jumuiya hiyo hutegemea kwa kiasi kikubwa na ushiriki wa wananchi katika hatua za mtanagamano huo kwani wao ndio walengwa wakuu katika mchakato huo.

Ni miaka 14 imepita tangu wakuu wa nchi za Afrika Mashariki waliposaini Mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na miaka 9 tangu kuanza kwa utekelezaji wa hatua ya kwanza ya mtangamano wa jumuiya hiyo. Pamoja na mafanikio ambayo Tanzania imeanza kuyapata kutokana na hatua mbalimbali za mtangamano wa jumuiya hiyo, inaelezwa kuwa bado mwitikio wa wananchi katika kuchangamkia fursa zilizopo uko chini.

Msemaji wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Vedastina Justinian anasema baada ya maandalizi ya miaka sita, nchi tano wanachama wa jumuiya hiyo zilianza kutekeleza rasmi hatua ya Umoja wa Forodha mwaka 2005.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...