JESHI la Polisi Mkoani Dodoma
linamshikilia Mwalimu wa Shule ya
Sekondari ya Hombolo Justus Jackson
(28) kwa tuhuma ya kumuua mwalimu
mwenzie kwa kukataa kulipa sh.
1,000 ya bili ya umeme aliyotakiwa
kuchangia marehemu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma,
David Missime amemtaja mwalimu
aliyeuwawa kuwa ni Freddy Ndahani
(29) mwalimu wa shule ya Hombolo.
Kamanda Misime amesema walimu hao wote
wawili wanalikuwa wakiishi katika
nyumba moja na walikuwa wakichangia
bili ya umeme katika nyumba hiyo.
Amesema katika mabishano walimu hao
waliingia katika ugomvi na inadaiwa Mwalimu Freddy alisukumwa katika ukuta na
kupoteza maisha papo hapo.
Kwa mujibu wa Kamanda Misime Mtuhumiwa huyo
ameshakamatwa na anatarajiwa
kufikishwa mahakamani mara baada ya
kukamilika kwa upelelezi.
Mambo gani haya? Kuua kama ilikuwa ni adhabu haiendani na kosa la kushindwa kulipa 1000,
ReplyDelete