Mtaalamu wa kujadili mikataba kutoka World Trade Organization (WTO), Prof. Dickson Yeboah akitoa mada jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa Kimataifa wa kuwajengea uwezo maofisa wa serikali kutoka nchi 15 za Afrika Mashariki, Afrika ya Kati na Afrika Kusini kuhusu uandikaji wa mikataba inayohusu Uwekezaji na Biashara. Mkutano huo umeandaliwa na Chuo Kikuu cha Bagamoyo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo.

Na Happiness Katabazi

CHUO Kikuu cha Bagamoyo (UB), kimesema kitaendelea kuandaa mafunzo  ya jinsi ya Kutengeneza mikataba na wawekezaji  kwa maofisa wa serikali za nchi zinazoendelea ili serikali hizo ziondokane na tatizo la kuandika mikataba ya uwekezaji ambayo haiziletei faida nchi zao.

Akizungumza na Katika  Mafunzo yanayoshirikisha wataaluma wa masuala ya Biashara toka nchi 15 yanayofanyika Katika Hotel ya Habour View Dar Es Salaam ambapo Mafunzo hayo yameandaliwa na Chuo Kikuu Cha Bagamoyo na kufadhiliwa na Chuo Kikuu Cha Nordic Africa Institute of the University of Uppsala Cha nchini Sweden, Mkuu wa Shule ya Biashara na Utawala (UB), Dk.Lenny Kasoga Alisema Mafunzo ya wiki mbili yameusisha  maofisa wa juu wa serikali mbalimbali ambao ni wataalamu wa fani ya Biashara toka nchi 15.

Dk.Kasoga alisema Leo Dunia ipo Karne  ya 21 lakini bado nchi  zinazoendelea ambazo  zimegundulika Kuwa na utajiri  mkubwa  zimejikuta zikiingia mikataba mibovu na wawekezaji KWA Sababu tu nchi hizo Hazina wataaluma serikalini ambao wamebobea Katika kufanya mijadala ya Kibiashara na wawekezaji na jinsi ya kuandika mikataba hiyo.

"Kwa kukuona tatizo Hilo sisi UB, tumeandaa Mafunzo haya ambayo yamewapa mwanga maofisa Hao waandamizi toka serikali za nchi 15 ambapo Mafunzo tuliyowapatia watayapeleka Katika serikali zao na vyuo vyao ili waweza kuandaa mitaala Katika vyuo vikuu vyao NGazi ya Shahada ya Pili ili watu wasome' Alisema Dk.Kasoga.

ALizitaja nchi zinazoshiriki Mafunzo ambayo ni ya kwanza kufanyika nchini  ambayo yanatarajiwa Kufungwa Ijumaa ya wiki hii na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk.Shukuru Kawambwa  Ni Mwenyeji Tanzania na Zanzibar, Madagascar,Mozambique, Rwanda,Malawi,Zambia, Burundi, Uganda, Ethiopia ,Kenya, Kongo, Malawi na Lesotho.

Kwa upande wake Profesa Francis Matambalya toka Chuo Kikuu Cha NAI, Uppsalla nchini Sweed, alisema chuo chao wameamua kufadhili UB iendeshe Mafunzo hayo kwasababu wanaamini UB ninauwezo wa kuendesha Mafunzo na kwamba Tanzania pia ambayo Katika Mafunzo hayo wamewasilisha na maofisa Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara nayo inamkabili na Changamoto hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Hivi ni kwa nini baadhi ya waandishe wetu huwa hampendi kutumia maneno au misamiati muafaka inayoendana sambamba na tukio au mazingira husika? Ni uhaba wa misamiati ya kiswahili au kutofaham maana zake. Nimesema hivyo kwa sababu ya hilo neno lililotumika hapo 'Kufunda' nadhani halikustahili hapo, japokuwa imeeleweka, lakini kwa uandishi na utumiaji wa maneno/misamiati ya kiswahili ulio fasaha, basi hapo si pahala pake, angalau lingetumika neno mathalan...Chuo kikuu cha Bagamoyo 'chawanowa' maofisa... lakini sio chawafunda... neno hilo lina mazingira yake na pahala pake maalum pa kulitumia na likakubalika zaidi kuliko lilivyotumiwa hapo.

    Samahani wahusika mana naamini baadhi yetu huwa wanakereka sana wanapokosolewa au kurekebishwa katika kazi zao.

    ReplyDelete
  2. Kweli mdau wa kwanza hapo juu yaani Globu ya Jamii imekuwa kama ''Magazeti- Pendwa''.

    Habari inayozungumzia shughuli ya maana kama hii inabidi iendane sawia na lugha/uandishi makini.

    Mdau
    Christos Papachristou
    Diaspora.

    ReplyDelete
  3. Ndugu HK

    Nashukuru kwa niaba ya UB na mwandishi wetu kwa ukosoaji wako wenye nia njema.

    Tutazingatia ushauri wako mzuri kila tutakapoandaa makala mengine juu ya mafunzo yetu ya kuwanoa maafisa na watu wengine.

    EGM

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...