Zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa limeendelea mkoani Mtwara, ambapo
wananchi wamejitokeza kwa wingi kujisajili, kama wakazi hawa wa Wilaya za
Tandahimba na Newala walivyokutwa wakishiriki kikamilifu kujisajili.
Moja ya changamoto kubwa iliyojitokeza ni wakazi wengi hususani maeneo ya
vijijini kukosa mashine za photocopy, huku baadhi wakikosa nyaraka muhimu
za kuwatambulisha. Changamoto nyingine ni waombaji wengi kutokuwa na
taarifa sahihi za umri wao binafsi na wazazi huku baadhi wakikosa taarifa
sahihi za maeneo wanakoishi.
Hata hivyo kwa maelekezo na mafunzo yaliyotolewa na NIDA kwa maafisa
wote wanaoendesha zoezi hilo changamoto nyingi zimeweza kutatuliwa
kutokana na miongozo na madodoso yanayomsaidia mwombaji kutambua
baadhi ya taarifa muhimu.
Hata hivyo NIDA imewaomba wananchi katika
maeneo mengine ambayo zoezi hili halijafanyika kuanza kujiandaa kwa
kuwa na nyaraka muhimu zinazoweza kuwatambulisha mathalani; cheti cha
kuzaliwa, kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, Cheti cha Elimu ya Msingi,
Sekondari au Chuo, Leseni ya Udereva, Kadi ya kupigia Kura, Pasipoti, Kadi ya
Bima ya Afya, nambari ya utambulisho ya mlipa kodi (TIN) pamoja na kuwa
taarifa sahihi zinazomhusu mwombaji binafsi na wazazi, majina, tarehe na
miaka ya kuzaliwa.
Kama kushereke siku za kuzaliwa hakupo ndiyo maana kumbu kumbu za tarehe ya kuzaliwa wanakuwa hawana.
ReplyDelete