Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandara akifungua mkutano wa mabadiliko ya tabianchi unaofanyika katika hoteli ya Kunduchi nje kidogo ya jiji la Dar Es salaam ukiwashirikisha watafiti na wanamazingira kutoka nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania.
Mkurugenzi wa kituo cha mafunzo ya mabadiliko ya tabianchi cha chuo kikuu cha Dar Es Salaam Profesa Pius Yanda akiwasilisha mada katika mkutano huo.
Profesa Mukandara akijadiliana na wataalam wanaoshiriki kwenye mkutano huo muda mfupi baada ya ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika Kunduchi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Wataalam wa mazingira na watafiti kutoka vyuo vikuu mbalimbali kikiwemo cho kikuu cha Dar es salaam na wadau wengine wa mazingira wanaohudhuria mkutano huo wa mabadiliko ya tabianchi katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Profesa Rwekaza Mukandara muda mfupi baada ya ufunguzi wa mkutano huo.Picha zote na Vedasto Msungu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...