Na: Geofrey Tengeneza
Taasisi na makampuni kadhaa yameendelea kujitokea kudhamini onesho la
kimataifa la utalii la Swahili ‘Swahili International Tourism Expo’ (SITE)
linaloandaliwa na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na ambalo linatarajiwa
kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City kuanzia Oktoba 1 – 4,
2014.
Aidha Bodi ya Utalii Tanzania imesema milango bado ipo wazi kwa makampuni
na taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kuwaunga mkono kwa kujitokeza
kudhamini onesho hili linalofanyika kwa mara ya kwanza.
Licha ya wadhamini wakuu wa onesho hilo ambao wako kiwango cha
platinum shirika la hifadhi ya taifa (TANAPA), mamlaka ya hifadhi ya eneo
la Ngorongoro (NCAA) pamoja na shirika la ndege la Ethiopia, wadhamini
wengine katika viwango vya dhahabu (Gold) na Silva (sliver) ni pamoja
Zanzibar collection, Hoteli za Sea Cliff, Serena hotel, Southern Sun, New
Africa, Hyatt Regency, Protea, Serena Bouganvillea Safari lodge, Acacia
Farm lodge na Soroi Tented Camp zimedhamini huduma ya malazi kwa
wageni maalumu ambao ni wafanya biashara wakubwa wa kusafirisha watalii
kutoka Marekani, Uingereza, Ujerumani n.k pamoja na wandishi wa habari wa
kimataifa wanaokuja kwa ajili ya onesho hilo.
Wakati Wizara ya mambo ya nje na Uhusiano wa kimataifa ikitoa udhamini wa
mabasi ya kubebea washiriki wakati wa onesho hilo, benki ya CRDB imetoa
udhamini wa fedha taslimu na inatarajiwa kuwa na banda ndani ya maonesho
hayo ya aina yake.
Kwa upande wa usafiri wa ardhini utadhaminiwa na makapuni Zara Tours,
Naeda Safaris Ltd, Wildlife Expedition Safari, huku Azam Marine wakijitokeza
kudhamini usafiri wa baharini kutoka Zanzibar. Mashirika ya ndege ya
Rwandair, Precision Air na Uturuki (Turkish airline) yatatoa tiketi za ndege kwa
ajili ya kuwasafirisha baadhi ya wageni wakati wa onesho hilo.
Makampuni mengine yaliyojitokeza ni yale yanayomiliki majarida. Haya ni
Event, Dar Life na 7th
Kenya,ambavyo vinatangaza onesho hili kupitia majarida yao.
Aidha kampuni ya Montage imetoa udhamini wa kuwa mpambaji katika kumbi
za mikutano. Boogie woogie pia wametoa udhamini na watakuwa na mgahawa
wao wa chakula katika banda la utalii wa utamaduni ilhali wadhamini wengine
Black Tomato wao watakuwa na banda la kuuza kahawa ya Tanzania.
‘Swahili International Tourism Expo’ litakuwa likifanyika kila mwaka mnamo
mwezi wa Oktoba na kuhudhuriwa na washiriki kutoka ndani na nje ya
Tanzania.
Floor Media kutoka hapa nchini na Go Places kutoka
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...