Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) wakianza matembezi ya hisani ya takribani Kilomita 10 jijini Dar es Salaam jana ikiwa ni moja ya matukio ya benki hiyo kudhimisha Siku ya Moyo Duniani ambapo kiasi cha pesa watakachochangisha kitapelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na matatizo ya ugonjwa wa moyo. Siku ya Moyo Duniani huadhimishwa kimataifa Septemba 29 kila mwaka.
Hapa baadhi ya wafanyakazi hao wakipita katika barabara ya Ocean Road kulekea maeoneo ya Coco Beach wakitokea makao makuu ya beni hiyo katika Tawi la Corporate, Posta Mpya.
Hapa ni daraja la Salender, kwa moyo wa kujitolea wafanyakazi hawa wa NBC wakiendelea na matembezi hayo ili kupata fedha kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo.
Safari inaendelea, hapa baadhi ya wafanyakazi hao wakikaribia kufika mwisho wa matembezi yao hapa ikiwa ni Barabara ya Kenyatta wakielekea Coco Beach.
Baada ya kumaliza matembezi hayo wafanyakazi hao wakipiga picha ya pamoja kuonyesha ushindi na mshikamano wao katika kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na matatizo ya magonjwa ya moyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...