Wadau mbalimbali wa madini ya vito waliopata bahati kutembelea Banda la Tanzania katika siku ya kwanza ya Maonesho ya 54 ya Kimataifa ya Vito na Usonara ya Bangkok, wakishangazwa na mng’ao wa Kito cha Tanzanite katika Pete iliyovalishwa kidoleni mwa Mwanafunzi, Raia wa Thailand aliyeomba kujaribisha Pete hiyo. Anayetoa maelezo ni Mfanyabiashara wa Madini ya Vito kutoka Tanzania, Bw. Gregory Kibusi (Mwenye mavazi ya Bhatiki).
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji wa Madini ya Almasi na Vito cha Wizara ya Nishati na Madini (TANSORT), Archard Kalugendo akizungumza na mdau wa madini ya vito aliyetembelea Banda la Tanzania. Kalugendo alitumia fursa hiyo kumkaribisha mdau huyo katika Maonesho ya Vito ya Arusha yanayotarajiwa kufanyika mwezi Septemba mwaka huu nchini Tanzania. Katikati ni Afisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Asimwe Kafrika.
Sehemu ya shehena ya madini mbalimbali ya vito katika Banda la Tanzania kwenye Maonesho ya 54 ya Kimataifa ya Vito na Usonara ya Bangkok.
Wafanyabiashara wa Madini ya Vito kutoka Tanzania, Gregory Kibusi (Mwenye nguo za Bhatiki) na Kassim Iddi Pazi (Mwenye Shati la rangi ya Bluu), wakimwonyesha Mteja aina mbalimbali za madini ya vito yanayopatikana Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...